.
22nd June, 2021
Shule moja iliyoko kaunti ya Nyandarua ambayo ilifungwa mapema wiki iliyopita baada ya wanafunzi 16 pamoja na walimu 4 kuthibitishwa wana virusi vya korona, itafunguliwa kwa wanafunzi wote wakati maafisa wa afya watadhibitisha kuwa wanafunzi hawako kwenye hatari ya kuambukizwa virusi hivyo shuleni humo. Kulingana na mshirikishi wa Nyandarua Benson Leparmorijo amesema shule hiyo imeanza kuwapokea wanafunzi kwa awamu, ikiwa tayari wanafunzi wa darasa la tano hadi saba wamerejea.