.
20th June, 2021
Maafisa wa polisi wamemuokoa msichana mwenye umri wa miaka 23 aliyetekwa nyara katika eneo la Makadara siku tano zilizopita na kumtia mbaroni mshukiwa mmoja anayedaiwa kuwa miongoni mwa watekaji nyara. Msichana huyo kwa jina Hafsa Mohamed alipatikana katika nyumba moja eneo la matopeni mtaa wa Kayole jijini Nairobi baada ya kuomba usaidizi kutoka kwa watoto waliokuwa karibu na nyumba hiyo.