19th June, 2021
Wazazi wana kila sababu ya kutabasamu baada ya serikali kupunguza karo ya shule za sekondari za umma kwa hadi shilingi elfu nane. Kwenye barua iliyoandikiwa wakurugenzi wa elimu katika kaunti, katibu wa elimu, Dkt Julius Jwan, amesema wizara ya elimu imechukuwa hatua hiyo kufuatia kupungua kwa mwaka mpya wa masomo kutoka thelathini na tisa hadi majuma thelathini.