.
16th June, 2021
Gavana wa Kirinyaga Ann Mumbi? Kamotho amejitenga na kauli ya kiongozi wa wengi bungeni, Amos Kimunya, aliyesema kwamba serikali haitatenga fedha za maendeleo kwa eneo bunge la Kiambaa endapo mgombea wa chama cha Jubilee hatochaguliwa. Gavana Mumbi amesema kwamba ni haki ya kila mkenya kutoa maoni yake katika taifa hili na kwamba hakuna yeyote anayepaswa kutishia au kuzima mitazamo ya wengine katika nchi inayojivunia demokrasia. Amesema kauli ya Kimunya ni yake binafsi na bali si msimamo wa chama cha Jubilee.