16th June, 2021
Kuna haja ya kuja na suluhu ya kudumu na mapendekezo ya kuimarisha na kulinda nyaya za mawasiliano ya kidijitali, simu na miundo msingi ya mawasiliano mingine ili isiharibiwe. Mwenyekiti wa kamati ya mawasiliano katika bunge la Seneti Gideon Moi, amesema kwamba wamekuwa wakipokea taarifa za uharibifu wa vifaa vya mawasiliano aiana hii kutoka kwa halmashauri ya mawasiliano nchini, jambo ambalo ni changamoto kwao. Moi alizungumza katika ufunguzi wa warsha iliowahusisha kamati yake, wizara ya mawasiliano na maswala ya vijana katika hoteli moja mjini mombasa. Warsha hio inaazimia kupokea mapendekezo ya kuhifadhi miundo mbinu ya mawasiliano ili ziwe madhubuti zaidi katika nyanja za mawasilino nchini na kimataifa.