.
16th June, 2021
Shule ya msingi ya Uhuru kaunti ya Nyandarua imefungwa kwa muda baada ya wanafunzi 16 na walimu wanne kupatikana na virusi vya Korona. Kwa mujibu wa waziri wa Afya katika kaunti hiyo John Mungai sampuli zilikusanywa kutoka shule hiyo baaada ya baadhi ya wanafunzi kuonesha dalili ya kuwa na virusi hivyo. Haya yanajiri huku waziri wa usalama wa kitaifa Dr. Fred Matiangi akisema kwamba huenda serikali ikaratibu vigezo vipya vya kudhibiti virusi vya korona katika eneo la magharibi na Nyanza.