12th June, 2021
Katibu mkuu wa jumuiya ya afrika mashariki, Dkt. Peter mathuki ambaye amekuwa ofisini tangu april 25 mwaka huu, amekutana na wakurugenzi watendaji wa makampuni ya biashara nchini Tanzania, katika hafla iliyofanyika jijini Dar es salaam, ikiwa ni mkakati wake wa kutatua kero linalokwamisha ustawi wa biashara baina ya nchi sita wanachama wa jumuiya ya afrika mashariki….hafla hiyo ya wakurugenzi watendaji iliyoandaliwa na baraza la biashara la Afrika mashariki (EABC), vyama vya biashara, viwanda na kilimo Tanzania na Zanzibar, inatazamiwa kuleta suluhu katika biashara baina ya nchi wanachama.