9th June, 2021
Familia moja katika eneo la Moi's Bridge kaunti ya Uasin Gishu inaishi kwa wasiwasi ya kumpoteza mwanao aliyekwenda kufanya kazi nchini saudi arabia baada ya mawasiliano kukatika kwa kipindi kirefu. Kutokana na ripoti za mateso na hata mauaji ya waafrika wanaokwenda uarabuni kufanya kazi sasa familia ya Jane Wamboi inahofia kwamba huenda maisha yake yamo hatarini.