9th June, 2021
Kampuni ya ndege Kenya Airways imeandikiana mkataba na shirikisho la mbio za magari duniani FIA kuboresha na kukuzaji vipaji kwa vijana katika makala ya mwaka huu ya WRC yatakayoandaliwa humu nchini mwezi huu. Afisa mkuu mtendaji wa mbio za magari za WRC Phineas Kimathi alidokeza umuhimu wa udhamini huo kwa ukuzaji wa vipaji zaidi katika mashindano haya ya magari kwa kuweka Kenya katika ramani ya dunia. Madereva hao walichaguliwa kutokana na weledi wao katika mashindano ya magari.