.
9th June, 2021
Mashahidi watatu katika kesi ya mauaji ya Tecra Muigai mwanawe mmiliki wa kiwanda cha kutengeneza vileo cha keroche sasa watatoa ushahidi wao faraghani. Hakimu Zainab Abdul ametoa agizo hilo baada ya upande wa mashtaka kutoa ombi hilo kwa kuhofia usalama wa mashahidi hao kwani wote ni wakazi wa lamu anakotoka mshukiwa mkuu Omar Lali ambaye alikuwa mpenzi wa Tecra. Omar alikamatwa na kuachiliwa huru mwezi julai mwaka jana baada ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma kumwondolea mashtaka ya mauaji.