.
5th June, 2021
Vikwazo vinazidi kuzikabili juhudi za kurekebisha katiba kupitia mchakato wa Bbi. Japo majaji saba wa mahakama ya rufaa wataanza kuisikiza kesi ya kupinga uamuzi wa majaji watano wa mahakama kuu walioharamisha mchakato mzima wa Bbi, rufaa nyingine imewasilishwa kuongezea uzito wa juhudi za kufutilia mbali Bbi. Hizi zinatishia dhamira yake Rais Uhuru Kenyatta kukuza utangamano wa taifa kupitia marekebisho ya katiba.