5th June, 2021
Kiongozi wa muungano wa wazee nchini Kung'u Muigai amewasuta vikali wazee kutoka baraza la wazee wa kikuyu walioshiriki zoezi la kusafisha hekalu la Mukurwe Wa Nyagathanga kufuatia kutawazwa kwa spika wa bunge la kitaifa Justin Muturi kama msemaji wa jamii ya Mlima Kenya. Akizungumza wakati wa hafla ya mazishi ya Rufas Rutere aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la wazee la Njuri Ncheke, Muigai amesema wazee hao ni wa kujitakia na kuwataka wakazi wa Mlima Kenya kuwapuuza. Viongozi wa kisiasa aidha wameunga mkono kutawazwa kwa Muturi.