2nd June, 2021
Kamati ya bunge la Seneti kuhusu Kawi, imemwagiza Waziri wa Kawi na Madini John Munyes kufika mbele yake mnamo tarehe 14 mwezi juni, la sivyo atatozwa faini au ilani ya kukamatwa itatolewa. Kulingana na mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Seneta wa Nyeri Ephraim Maina, lengo kuu la kikao hicho ni kujadili suala la kuongezwa kwa bei ya mafuta katika miezi ya hivi karibuni.