2nd June, 2021
Katika hotuba yake ya sherehe za madaraka hapo jana akiwa Kisumu, Rais Uhuru Kenyatta alitoasemi kadha kuhusu uchumi ambazo zililenga kuipigia debe serikali yake. Lakini baadhi ya kauli hizo sasa zinatiliwa shaka. Baadhi ya yale aliyogusia ni ikiwemo kuimarika kwa uchumi maradufu tangu achukue hatamu za uongozi. Hata hivyo, alidokeza kwamba, baada ya mahakama kuharamisha uchaguzi mkuu wa 2017, Kenya ilipoteza shilingi trilioni moja ndani ya siku 123 baada ya uamuzi huo. Je, kuna ukweli ndani ya maneno hayo?