.
2nd June, 2021
Vikao vya kusikiliza kesi ya rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama kuu kuharamisha mchakato wa marekebisho ya katiba kupitia mswada wa BBI vitaanza tarehe 29 mwezi huu na kukamilika tarehe mbili mwezi ujao wa Julai. Katika kikao cha kutathmini maswala yanayohusu kesi hiyo rais wa mahakama ya rufaa daniel musinga amesema majaji saba wa mahakama hiyo watasikiliza na kutoa uamuzi kuhusu kesi hiyo akiwaonya wahusika kukoma kuizungumzia nje ya mahakama.