.
1st June, 2021
Hatimaye miili ya pacha ambao walifariki baada ya kuzama wakiogelea katika ufuo wa gasi eneo la Msambweni kaunti ya Kwale imepatikana. Pacha hao Kennedy Gichui na nduguye Solomon Macharia wa miaka 18, walitoweka hapo jana na miili yao kupatikana ikielea mapema leo na waogeleaji wa kaunti. Kulingana na waogeleaji hao wakiongozwa na Clara Mulwa marehemu walikuwa wamekumbatiana kuashiria kwamba walitaka kutoka majini pamoja ili kukwepa mauti. Kulingana na baba yao Samuel Njuguna, pacha hao walikuwa wanasubiri kujiunga na taasisi za elimu ya juu.