×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Mili ya pacha waliozama ufuo wa gesi eneo la Msambweni, Kwale imepatikana hii leo

1st June, 2021

Hatimaye miili ya pacha ambao walifariki baada ya kuzama wakiogelea katika ufuo wa gasi eneo la Msambweni kaunti ya Kwale imepatikana. Pacha hao Kennedy Gichui na nduguye Solomon Macharia wa miaka 18, walitoweka hapo jana na miili yao kupatikana ikielea mapema leo na waogeleaji wa kaunti. Kulingana na waogeleaji hao wakiongozwa na Clara Mulwa marehemu walikuwa wamekumbatiana kuashiria kwamba walitaka kutoka majini pamoja ili kukwepa mauti. Kulingana na baba yao Samuel Njuguna, pacha hao walikuwa wanasubiri kujiunga na taasisi za elimu ya juu.

.
RELATED VIDEOS