.
1st June, 2021
Kumeshuhudiwa purukashani, mbwebwe na vioja katika sherehe za mwaka huu za madaraka katika uga wa Jomo Kenyatta mjini Kisumu. Ilibidi polisi kutumia gesi ya kutoa machozi kuwatawanya wakazi wa mtaa wa Kondele waliokuwa wakiandama msafara wa Rais Uhuru Kenyatta akielekea katika eneo la mkutano. Ndani ya uwanja wa mkutano afisa wa jeshi la wanamaji alizirai kwenye gwaride na afisa mwingine wa jeshi la wanahewa akikosa kutua kwa parachuti ilivyotayarajiwa na kujeruhiwa vibaya. Katika kioja kingine mwanamume mmoja alibebwa hobela hobela na maafisa wa usalama alipojaribu kukimbia na kumkaribia Rais Uhuru Kenyatta.