.
29th May, 2021
Spika wa bunge la kitaifa Justin Muturi amejitokeza waziwazi kutetea wazee wa jamii ya Kikuyu dhidi ya shutuma dhidi yao na baadhi ya magavana na viongozi wa kisiasa kutoka eneo la Mlima Kenya. Muturi anasema wajibu wa wazee wa kijamii umelindwa na katiba. Akizungumza wakati wa mkutano wa muungano wa wasomi kutoka eneo la Meru, Muturi amewataka kumuunga mkono katika azma yake ya kuunganisha eneo hilo na taifa kwa jumla. Viongozi waliozungumza aidha wakiahidi kusukuma ajenda hiyo.