23rd May, 2021
Wakaazi wa kaunti ya Vihiga wameanzisha mchakato wa kukusanya saini kumtaka kisheria Rais Uhuru Kenyatta kuivunjilia mbali serikali ya kaunti hiyo kwa kuwa imeshindwa kutekeleza majukumu yake na kuwarejesha nyumbani wawakilishi wote wa bunge la kaunti hiyo. Wakaazi hao wanasema gavana wa kaunti hiyo Daktari Wilber Otichilo ameshindwa kutekeleza majukumu yake na wawakilishi wadi wametiwa mfukoni.