.
22nd May, 2021
Naibu Rais William Ruto kwa mara nyingine ameanza safari ya kutaka uungwaji mkono katika eneo la Pwani katika uchaguzi mkuu ujao. Katika kikao na wabunge wa Pwani wanaoegemea mrengo wake pamoja na wasomi Ruto aliyeepuka kuzungumzia siasa ameonekana kuvumbua mkondo tofauti kabisa katika kuwavutia wapiga kura. Katika kikao cha leo kilichoandaliwa kaunti ya Kilifi kuzungumzia uchumi wa Pwani wabunge walimtaka kuhakikisha matakwa yao yametimizwa kabla ya kumpigia kura.