15th May, 2021
Mwaka wa 1997 serikali iliagiza kipande cha ardhi kutoka kwa wakazi wa eneo la Chebara kaunti ya Elgeyo Marakwet ili kutengeneza bwawa la maji lilolenga kusambaza maji mjini eldoret na badala yake ikaahidi kutengeneza shule katika maeneo hayo.mnamo 2011 serikali ikatenga shilingi milioni 635 kufanikisha miradi katika shule ya upili ya wavulana na wasichana ya Chebara. Ila miaka michache baadaye taswira ya majengo yalioachwa pasi kukamilishwa yanaatua moyo hata baada ya mamilioni ya pesa kutumika.