.
15th May, 2021
Siku chache baada ya katibu mkuu wa chama cha walimu KNUT kupata pigo mahakama ilipoidhinisha kuondolewa kwake kwenye sajili ya walimu, kundi moja chini ya mwavuli 'Team Change' limesema liko tayari kuchukua hatamu za uongozi kutoka kwake Sossion. Kwenye msafara mpya ambao umezinduliwa baada ya mkutano na wajumbe wa KNUT uliofanyika mjini Eldoret, Henzry Oyuu kutoka eneo la nyanza anapigiwa upatu kuwania nafasi ya katibu mkuu huku Rosalia Nkajala kutoka Pwani akipaniwa kuwania nafasi ya Naibu Katibu Mkuu.