13th May, 2021
Juhudi za gavana wa wajir, mohammed abdi muhamad za kutaka kujua chanzo cha stakabadhi za benki zinazomhusisha mke na watoto wake kwenye sakata ya ufujaji wa pesa za kaunti ya wajir ziligonga mwamba mbunge wa wadi ya diff, shueb bare ahmed alipokataa kufichua vyanzo vyake. gavana abdi anasema hoja ya kutaka afurushwe afisini imechochewa na mahasidi wake na akakanusha madai kwamba amemuachia mke wake, kheira omar, majukumu ya kuendesha serikali ya kaunti. aidha, mfanyabiashara osman abdi jimale, anayedaiwa kuwa jamaa wa karibu wa mke wa gavana, hakufika mbele ya seneti kueleza jinsi makampuni anayomiliki yalifaidi zabuni kwenye kaunti.