.
12th May, 2021
Wizara ya afya imetoa ufafanuzi kuwa kaunti zilizo na idadi ya chini ya wale wanaopokea chanjo watapewa usaidizi wa kusambaza chanjo hio huku chanjo hizo zikisemekana kuharibika ifikapo tarehe 28 mwezi juni. Serikali aidha imeweka mikakati ya kupokea chanjo milioni 30 kutoka kampuni ya Johnson and Johnson ili kuchanja idadi ya wale waliosalia. Aidha idadi ya wale waliopatikana na aina ya korona kutoka india pia imeongezeka.