.
10th May, 2021
Washikadau wa utalii katika kaunti ya kilifi wanadai wametengwa kwenye mipango ya chanjo ya COVID-19. Wanasema wamekuwa wakishangazwa na hatua ya kutochanjwa licha ya kuwa wao wanatangamana na wageni kutoka mataifa mbalimbali. Wakizungumza huko malindi katika hafla ya usafi ya kila mwezi inayoandaliwa na progressive welfare association of malindi, wamesema wenzao kutoka kaunti ya nairobi na mombasa tayari wamechanjwa ila hawaelewi kwa nini shughuli hiyo upande wao haijang'oa nanga.