25th April, 2021
Baadhi ya viongozi kutoka magharibi ya Kenya wanaoegemea upande wa gavana wa kaunti ya Kakamega Wycliff Oparanya sasa wanashurutisha sharti gavana huyo apewe tiketi ya ugombezi urais wa chama cha Odm la sivyo atagura kuelekea vyamani vingine vya kisiasa. Viongozi hao wanasema ni wazi kuwa Oparanya anapania kufanya kazi na viongozi wengine baada ya kukutana na Naibu Rais William Ruto na kiongozi wa wiper Kalonzo Musyoka. Oparanya kwa upande wake amesisitiza kuwa zamu imewadia kwa kiongozi wa odm Raila Odinga kumlipa deni kwa kumuunga mkono.