.
25th April, 2021
Wanahabari wawili wa shirika la Standard ni miongoni mwa waandishi walioachiliwa huru kutoka kituo cha polisi cha Matuu bila kufunguliwa mashtaka baada ya kukamatwa na kuzuiliwa wakiripoti kuhusu zoezi la kubomoa nyumba na kuwatimua wakaazi kutoika ardhi ya shirika la TARDA eneo la Makima kaunti ya Embu. Mbunge maalum Cecil Mbarire amelaani kisa hicho cha wakaazi wa eneo hilo kutimuliwa katika ardhi yao akitaka serikali kutafuta suluhu ya mgogoro huo mara moja.