.
25th April, 2021
Ni mwanasayansi, mhadhiri na msomi ambaye ametuzwa kama mwanamke bora zaidi barani Afrika na nchi za kiarabu kwenye tuzo ya kimataifa kuwatambua wanawake waliobobea kwenye sayansi maarufu kama Loreal Unesco mwaka wa 2021. Catherine Ngila mwenye umri wa miaka sitini ni miongoni mwa wanawake watano bora zaidi kote ulimwenguni juhudi zake kwenye sayansi ya usafi wa maji zikimwezesha kuibuka mshindi. Katika makala ya mwanamke ngangari leo hii tunamwangazia mama huyo ambaye angali na kiu ya kuendelea na utafiti wa sayansi ya maji.