.
21st April, 2021
Tanzania inatarajia kuanza kutumia reli yake ya kisasa (SGR) inayotumia umeme, mapema mwezi Agosti mwaka huu, katika kusafirisha abiria na mizigo kuanzia mjini dar es salaam hadi morogoro, umbali wa kilometa 205. Ikiwa ni kipande cha kwanza cha reli hiyo inayotarajiwa kufika hadi kwenye fukwe za ziwa Victoria mjini mwanza, ili kuunganisha taifa hilo na nchi jirani za Uganda, Burundi, Rwanda na DRC. Reli hiyo itakayokuwa na urefu wa kilometa zaidi ya 1,219 inakuwa ya kwanza afrika mashariki.