.
21st April, 2021
Shughuli ya kurekebisha katiba kupitia mchakato wa BBI imeingia baada ya jopo la wataalam waliochambua mswada huo kufichua dosari kadhaa. Kamati ya pamoja ya bunge la taifa na bunge la seneti imegundua kwamba huenda ni kaunti 13 pekee zilizojadili mswada halisi wa BBI, ilhali mabunge mengine ya kaunti yalijadili miswada ghushi. Aliyekuwa katibu wa jopo kazi lililoshughulikia mchakato wote wa bbi kabla mswada huo kuwasilishwa kwa tume ya IEBC amesema huenda watu fulani wamepanga njama ya kuhujumu shughuli hiyo na akatoa wito kwa idara ya upelelezi kuingilia kati.