.
21st April, 2021
Waziri wa afya Mutahi Kagwe amesema kuwa mpango wa kuagiza chanjo aina ya Pfizer Na Johnson & Johnson unaendelea, kama njia mbadala ya kutimiza mpango wa kuwachanja wakenya kutokana na virusi vya korona. Waziri Kagwe ameonya kuwa licha ya maambukizi ya virusi vya korona kupungua katika kaunti zilizoorodheshwa kama hatari zaidi, maambukizi yanaongezeka katika kaunti nyinginezo.