21st April, 2021
Huenda walimu ishirini na saba wakaadhibiwa kwa kupigwa kalamu kufuatia madai ya kuhusika kwenye udanganyifu wa mtihani wa KCSE ambao umekamilika hii leo. Waziri wa elimu Profesa George Magoha, amesema watu wengine 37 wakiwemo wafanyabiashara na wanafunzi wa vyuo vikuu walihusika kwenye udanganyifu wa mtihani wa KCSE.