×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Deni la Karo: Mwanafunzi aliyezuiliwa baada ya KCSE kwa deni la karo ya shilingi 9,000 aachiliwa

20th April, 2021

Saa chache za mahangaiko kwa mwanafunzi mmoja wa shule ya sekondari ya wasichana ya St. Georges Grasslands katika kaunti ya Nakuru zimekamilika mapema leo hii baada ya kupata fursa ya kuelekea nyumbani kwao likoni, kaunti ya Mombasa. Mwanafunzi huyo aliyekamilisha mtihani wake wa kidato cha nne (KCSE) hapo jana, alidaiwa kuzuiliwa na usimamizi wa shule iyo kuondoka baada ya wazazi wake kukosa kukamilisha deni la karo ya shilingi elfu tisa. Ilimlazimu binti huyo kutoroka shuleni na kutafuta pa kulala kutoka kwa wasamaria wema kabla ya kupata njia ya kusafiri, lakini anavyoarifu mwanahabari wetu Ibrahim Karanja usimamizi wa shule hiyo umekataa kata kata kwamba ulimzuia mwanafunzi huyo kuondoka shuleni.

 

.
RELATED VIDEOS