.
7th April, 2021
Baraza la Magavana limetangaza kuwepo kwa takriban viwanda 58 vinavyotengeneza gesi aina ya Oxygeni katika kaunti 47, ila inaongezea kwamba ni viwanda arobaini na viwili pekee ambavyo vinatengeneza gesi hiyo kwa sasa. Vilevile baraza hilo limetoa wito kwa kaunti kuripoti iwapo watakumbana na changamoto ya upungufu wa gesi hiyo ambayo imeshuhudiwa katika hospitali kuu ya kenyatta na kuilazimu hospitali hiyo kupiga marufuku shughuli ya upasuaji wa wagonjwa usiokuwa wa dharura.