.
2nd March, 2021
Je huenda naibu rais William Ruto akafurushwa kutoka kwa chama cha Jubilee? Ndilo swali vinywani mwa wakenya, baada ya mwandani wake kisiasa Caleb Kositany kupokonywa wadhifa wa naibu katibu mkuu wa chama cha Jubilee, na kukabidhiwa mbunge wa Cherangany Joshua Kutuny.