.
1st March, 2021
Wenyeji wa wa kijiji cha Muthure katika eneo bunge la Kabete kaunti ya Kiambu wameelezea mshangao wao baada ya mti wanaouthamini kwa mujibu wa itikadi zao, kuanguka. Mti huo wauitao Mugumo ulianza kwa kunyauka matawi yake na kisha wazee kuandaa tambiko chini yake, ila sasa mti wenyewe umeng'ooka na kuanguka. Wakazi hao wanadai lipo jambo fiche ambalo wangependa wazee wawafafanulie kuhusu kuanguka kwa mti huo.