.
1st March, 2021
Mgawanyiko umetokea katika familia ya mbunge wa zamani wa Matungu Justus Murunga aliyefariki mwishoni mwa mwaka jana na kutoa nafasi kwa kiti cha ubunge cha Matungu. Mkewe Christabel Murunga na mwanawe Eugine Murunga wanagombea ubunge huo hatua ambayo imetishia kuisambaratisha familia hiyo.