.
26th February, 2021
Naibu mwenyekiti wa chama cha jubilee David Murathe ametangaza kwamba mikakati ya kumtimua naibu rais William Ruto kutoka makazi yake rasmi ya serikali huko Karen inakaribia kukamilika. Lakini kwa upande wake, Ruto ambaye anazidi kuwindwa na chama chake amesema yuko tayari kupambana na wapinzani ana kwa ana. Ktn news imethibitisha kwamba mwenyekiti wa kamati ya taifa simamizi ya chama hicho NMC ameandaa mkutano siku ya jumatatu wa kumfurusha caleb kositany kama naibu katibu mkuu wa Jubilee