25th February, 2021
Chama cha ODM kimeahirisha tarehe ya mwisho ya kuwasilisha maombi ya kuwania urais mwaka 2022 kutumia tiketi yake. Miongoni mwa wale walioeleza azma ya kupeperusha bendera ya urais chamani humo ni gavana wa Mombasa ali hassan joho na gavana wa kakamega wycliffe oparanya. Ingawa kinara wa odm raila odinga hajaweka bayana azma ya urais, hapo jana alitoa dalili kuhusu kile atakachofanya kuhusu mgao wa fedha wa kitaifa kupitia mswada wa BBI.