17th February, 2021
Familia ya watoto pacha waliotenganishwa katika hospitali ya rufaa ya kakamega wanaoishi katika eneo bunge la likuyani kaunti ya kakamega na kisha kupatikana miaka 19 baadaye, sasa inadai kupitia hali ngumu ya maisha licha ya wahisani kadhaa kujitokeza kugharamia masomo ya watoto hao na mahitaji mengine muhimu.Mevis mbaya melon lutenyo na sharon mathias ambao wanatarajiwa kufanya mtihani waowa kidato cha nne kcpe mwezi mei, wamekuwa wakipitia hali ngumu ya maisha masomo yao yakitatizwa baada ya wahisani wote waliojitokeza kuwasaidia takriban miaka miwili iliyopita kukosa kutimiza ahadi zao.