.
11th February, 2021
Mfumo mpya wa elimu unakusudia kubadilisha kabisa masomo nchini kenya. Kwa mujibu wa ripoti ya jopokazi la utekelezaji wa mtaala mpya wa masomo, CBC, mitihani haitatumika tena katika kuwatathmini wanafunzi katika kutoa mwelekeo wa taaluma na elimu ya mtoto. Hata hivyo walimu, wanafunzi na wazazi watahitajika kushirikiana pakubwa.