11th February, 2021
Shughuli ya kuwateua vijana wanaotaka kujiunga na jeshi limeng'oa nanga hii leo katika kaunti ndogo ya kwanza huku kukishuhudiwa idadi kubwa ya vijana waliojitokeza. Luteni kanali Gilbert Gichuhi alihakikishia umma kwamba shughuli hiyo itaendeshwa kwa njia ya usawa na haki huku akionya wale wanaokusudia kupeana hongo kwamba watachukuliwa hatua za kisheria wakipatikana, alikitaja kisa kimoja ambacho kijana mmoja alipatikana na stakabadhi gushu ambapo alipeanwa kwa polisi ili wamfungulie mashtaka. shughuli hiyo itaendelea katika kaunti ndogo za transnzoia west ,endebess,kiminini na cherengany ikikamilika tarehe 18 mwezi huu katika kaunti nzima ya transnzoia.