9th February, 2021
Aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Mbuvi Sonko ameachiliwa kwa dhamana ya shillingi laki tatu. Hii ni kwenye kesi kumi za kuwajeruhi watu pamoja na wizi wa kimabavu. Hakimu stella atambo alitoa uamuzi huo akitofautiana na upande wa mashataka. Hakimu atambo alisema kuwa Sonko ni mtu anayejulikana na hakuna sababu uyoyote ya kueleza ni kwa nini upande wa mashtaka ulimuona kama anayeweza kutorokea nje ya nchi, mahakama ilipinga vilevile sababu zilizotolewa na upande wa mashtaka. Baadaye Sonko alifulilizwa hadi mahakama ya Kahawa West ambapo anaandamwa na kesi ya kigaidi. Mahakama hiyo iliombwa kuairisha kesi hiyo ilikumruhusu Sonko kupata matibabu.