.
9th February, 2021
Chama cha Jubilee kimemtimua kiranja wa wengi bungeni Irungu Kang’ata na kumpa seneta wa Kiambu Kimani Wamatangi nafasi hiyo. Kang’ata alijipata taabani kuanzia mwanzo wa mwaka huu baada ya barua aliyomwandikia rais kuhusu mchakato wa mageuzi ya katiba kuibua hisia na hoja ambazo chama hakikufurahishwa nazo. Jubilee inamlaumu Kanga'ta kwa kutoboa siri za chama.