3rd February, 2021
Aliyekuwa gavana wa nairobi mike sonko alishindwa kujizuia na kulia mahakamani alipofika kujibu kesi ya ubadhirifu wa shilingi millioni 14. Sonko alimuambia hakimu wa mahakama ya kuskiza kesi za ufisadi douglas ogoti kuwa polisi walimwekelea mashtaka ya jinai baada ya yeye kumtaja dadake Rais Uhuru Kenyatta, Christine Pratt katika taarifa yake kwenye harakati ya uteuzi wa naibu gavana wa Nairobi. Mawakili wa Gavana huyo wa zamani wakiongozwa na daktari John Khaminwa waliomba korti muda wa mwezi mmoja ili kujiandaa kwa kesi hiyo japo mahakama imewapa mawakili hao wiki mbili tu kujiandaa. Sonko alihadithia mahakama jinsi alivyoteswa katika kituo cha polisi cha Gigiri.