28th January, 2021
Familia moja mjini Embu imelazimika kuigeuza nyumba yao kuwa chumba cha matibabu kufuatia gharama ya juu ya matibabu hospitalini. familia ya elias nthiga inasema mtoto wao mwenye umri wa miezi minane aligunduliwa kuwa na mashimo mawili kwenye moyo wake akiwa na umri wa miezi mitatu na kwamba wanahitaji shilingi milioni moja na nusu kumpeleka kwa matibabu nchini india. hata hivyo kama njia ya kupunguza kuongezeka kwa gharama ya matibabu katika hospitali ya rufaa ya kenyatta alikotibiwa mtoto huyo, wahudumu wa afya wamewashauri kununua mtungi wa gesi na vifaa vingine vya matibabu wanaposubiri kupata fedha za kutosha kumsafirisha mtoto wao wa kike kwa matibabu zaidi.