27th January, 2021
Kizaazaa kilishuhudiwa mtaani kayole hapa jijini nairobi baada ya jamaa aliyekuwa akitafutwa na polisi kwa madai ya kumuuwa mpenziwe eneo la kasarani wiki jana, kutishia kujitoa uhai maafisa wa polisi walipomfumania nyumbani kwake kwenye orofa ya tano. haya yanajiri huku polisi wakianzisha uchunguzi kubaini chanzo cha moto uliosababisha vifo vya watoto wawili katika mtaa huo wa kayole.