.
19th January, 2021
Waziri wa usalama wa ndani Fred Matiang'i amesema kwamba serikali inachukulia kwa uzito matukio ya huko Kapedo na kwamba utovu wa usalama unaoshuhudiwa yamkini unafadhiliwa na wanasiasa fulani, na kwamba hatua itachukuliwa. Amezungumza hapa Nairobi mapema leo baada ya kukutana viongozi wa kaskazini mashariki ya Kenya.