16th January, 2021
rais yoweri kaguata museveni ametangazwa kuwa mshindi katika uchaguzi mkuu wa uganda kwa kupata kura milioni 5.8. mpinzani wake robbert kyagulanyi anayejulikana kama bobi wine kwa jina la usanii amekuwa wa pili kwa kura milioni 3 nukta nne. hii ina maana museveni anachukua muhula mwingine wa miaka sita na tayari ameongoza nchini kwa miaka 35. bobi wine amekataa kutambua matokeo hayo akisema kuwa uchaguzi ulikumbwa na udanganyifu mkubwa akilaumu chama cha nrm kwa kutumia mabavu