.
13th January, 2021
Posta Rangers walipoteza fursa ya kuvuna alama tatu muhimu kwenye ligi kuu ya soka nchini baada ya kutoka sare ya bao moja kwa moja dhidi ya Zoo Kericho. Collins Neto aliifungia zoo bao la kwanza dakika 42 kabla ya Dennis Oalo kusawazisha dakika ya 68. Posta walipoteza tuta la penalti katika dakika ya 20.